Monday, August 18, 2008

Rushaka basi Olimpiki

MUOGELEAJI wa Tanzania, Khalid Yahya Rushaka jana alishika nafasi ya tatu kwenye michuano ya awali ya kuogelea lakini akashindwa kusonga mbele baada ya kumaliza mchezo wa mita 50 akiwa nje ya muda unaotakiwa.

Rushaka, ambaye alishiriki mchezo wa kuogelea wa mita 50 (freestyle) alitumia muda wa sekunde 28.50 ambao ni tofauti ya sekunde 7.04 wa muda wa kufuzu kwenda raundi ya pili na hivyo kutupwa nje ya mashindano hayo.

Kwa mujibu wa tovuti ya Olimpiki, Rushaka alishiriki mchuano wa mchujo akiwa Kundi la tatu na akashika nafasi ya tatu akiwa nyuma ya muogeleaji wa Malawi, Charlton Nyirenda, aliyetumia sekunde 27.46 na Jackson Niyomugabo wa Rwanda aliyetumia sekunde 27.74.

Kundi hilo halikuweza kutoa muogeleaji wa kwenda raundi ya pili baada ya wote kuwa chini ya muda wa kufuzu.


No comments: