Wednesday, September 24, 2008

Mawaziri 10 Waondoka Na Mbeki


Mawaziri 10 katika serikali ya Afrika Kusini wamejiuzulu, hatua hiyo inatokana na kung'olewa madarakani kwa rais Thabo Mbeki na chama tawala cha African National Congress.

Miongoni mwao ni waziri wa fedha, Trevor Manuel anayesifika kwa kuimarisha uchumi wa nchi hiyo.

Wengine ni mawaziri wa ulinzi, usalama na ujasiriamali wa umma.Barua zao za kujiuzulu zimeidhinishwa na Bw Mbeki mwenyewe ambaye bado hajaondoka rasmi madarakani.

Kujiuzulu kwa makamu wa rais Bi Phumzile Mlambo-Ngcuka kulitangazwa mapema, naye akichukua hatua hiyo kumfuata rais Thabo Mbeki.

Kiongozi huyo aliyeng'olewa na chama chake hata hivyo amenukuliwa akisema atafungua kesi kupinga uamuzi wa mahakama kwamba aliingilia kesi dhidi ya Jacob Zuma.

No comments: