Monday, September 29, 2008

17 Walipuliwa Syria


Serikali ya Syria imesema takriban watu 17 wameuawa na wengine 14 kujeruhiwa katika shambulio la bomu lililotegwa ndani ya gari nje ya mji mkuu, Damascus.

Eneo lililokusudiwa kulipuliwa bomu hilo halijajulikana lakini limelipuka karibu na msikiti mmoja wa madhehebu ya Shia na kituo kimoja cha usalama.

Mashambulio kama hayo ni nadra sana kutokea nchini humo.

Mlipuko huo unaonekana kuwa tishio kubwa kabisa kwa usalama wa taifa hilo kutokea katika kipindi cha miaka mingi iliyopita.

Waziri wa mambo ya ndani wa Syria, Jenerali Bassam Abdel Majid, ameelezea shambulio hilo kuwa la kigaidi.

Hata hivyo amekataa kusema ni nani anayehusika na shambulio hilo.

Televisheni ya Syria ilisema gari lililokuwa na mabomu yenye kilo 200 lililipuliwa karibu na kituo cha usalama cha ukaguzi wa magari katika barabara inayoelekea uwanja wa ndege nchini Syria.

No comments: