Monday, September 29, 2008

Wamarekani Wawakaribia Maharamia

Meli ya kivita ya Marekani imefanya mawasiliano na meli ya Ukraine iliyokamatwa na maharamia wa kisomali wiki iliyopita iliyotia nanga karibu na bandari ya Dobyo.

Hakuna ishara zozote kuonyesha kuwa meli hiyo ya Marekani ya USS Howard inaikaribia meli ya MV Faina iliyobeba vifaru vya kivita 33 aina ya T-72.

Meli hiyo ya MV Faina ilikuwa ikielekea nchini Kenya.

Meli nyingine ya kivita ya kirusi nayo inaelekea katika eneo hilo.

Maharamia hao wameripotiwa kudai fidia ya dola za kimarekani milioni 35 ili kuiachia huru meli hiyo ya Ukraine na mabaharia wake.

Hata hivyo, serikali ya Kenya imeonyesha wasiwasi juu ya ripoti hiyo ikisema kuwa hakukuwepo na taarifa za kutaka kulipwa fidia.

Maharamia hao pia walitoa onyo dhidi ya jitihada zozote za kuokoa mabaharia na meli hiyo.

No comments: