Monday, September 22, 2008

ANC Kupendekeza Rais wa Mpito


Chama Tawala nchini Afrika ya Kusini, kimesema kinatarajia kutoa jina la Rais wa mpito baadae leo, baada ya chama hicho kumlamzimisha Thabo Meki kujiuzulu.

Baleka Mbete ambaye ni spika wa nchi hiyo, ana nafasi kubwa katika chama hicho kupata nafasi ya kuwa rais wa mpito mpaka hapo mwakani kutakapo fanyka uchaguzi mkuu.

ANC kinamshinikiza Bw. Mbeki kujiuzulu kutokana na kile kinachosemekana kuwa alikuwa akishinikiza Bw. Zuma kuhukumiwa kutokana na kesi ya ufisadi iliyokuwa ikimuandama. Lakini jaji mmoja wa nchini humo aliifutilia mbali kesi ya Bw. Zuma na kusema huenda kulikuwa na maswala ya kisiasa katika kesi hiyo. Bw. Mbeki amekana shutuma hizo na kusema anaheshimu uamuzi wa chama cha ANC.

No comments: