Sunday, September 21, 2008

Chakula Afrika Mashariki Mgogoro


Umoja wa Mataifa umesema takriban watu milioni 17 katika pembe ya Afrika wanahitaji chakula cha dharura na misaada mengine mara mbili ya ilivyotakiwa hapo awali.

Umoja huo umesema kiasi cha dola za kimarekani milioni 700 zinahitajika kwa ajili ya msaada huo wa dharura ili kuzuia hali hiyo isiongezeke.

Afisa mwandamizi wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya kibinadamu, John Holmes, amesema akiba ya chakula imepungua sana katika maeneo ya Ethiopia, Somalia, Eritrea, Uganda na kaskazini mwa Kenya.

Maeneo hayo yameathirika sana na ukame, migogoro na kupanda kwa bei za vyakula.

Bw Holmes amesema, " Huku hali ya ukame ikiongezeka na msimu wa njaa ukiendelea" idadi ya watu watakaoathirika inaweza kuongezeka.

Inakadiriwa kuhitajika jumla ya bilioni za kimarekani 1.4 ili kusaidia watu wanaohitaji msaada kwa mwaka huu peke yake.

Bw Holmes amesema takriban nusu ya idadi hiyo imepatikana lakini kuna upungufu wa dola za kimarekani milioni 716.

No comments: