Friday, September 26, 2008

Motlanthe Awa Rais wa Mpito Bondeni


Naibu kiongozi wa chama tawala cha African National Congress cha Afrika Kusini Kgalema Motlanthe ameapishwa kuwa rais wa muda nchini humo.

Bwana Motlanthe anachukua nafasi ya Bwana Thabo Mbeki aliyejiuzulu wiki iliyopita baada ya chama chake mwenyewe kusisitiza afanye hivyo.

Bw Montlanthe ameshinda robo tatu ya kura za siri zilizopigwa katika bunge la nchi hiyo mjini Cape Town.

Hata hivyo kulikuwa na zaidi ya kura arobaini zilizoharibika.

Trevor Manuel ambaye ni waziri wa afya anayeheshimika sana nchini humo ameshikilia nafasi yake licha ya kutaka kuachia ngazi.

Kujiuzulu kwa Bw Mbeki kulisababisha mawaziri wengi wa nchi hiyo kujiuzulu.

Bw Manuel alikuwa ni mmoja kati ya wawakilishi 11 wa bunge hilo kujiuzulu lakini amesema ameridhika kumtumikia rais mpya.

Mothlante alichukua nafasi ya naibu rais wa chama tawala cha ANC mwaka jana akiungwa mkono na Jacob Zuma.

Bw Zuma ambaye ndiye kiongozi wa chama hicho anatarajiwa kuwa rais wa nchi hiyo katika uchaguzi unaofanyika mwakani.

1 comment:

Anastácio Soberbo said...

Hello, I like this blog.
Sorry not write more, but my English is not good.
A hug from Portugal