Sunday, September 28, 2008

Obama Amshinda McCain Kwenye Mdahalo


Maoni ya papo kwa hapo yaliyopokelewa na kituo cha televisheni cha CNN pamoja na kituo cha utafiti wa maoni cha Opinion Research Corp yameonesha Bwana Obama alipata asilimia 51 wakati Mc Cain alama zake zilikuwa asilimia 38.

Hata hivyo pande zote zimedai kupata ushindi katika mdahalo huo, huku upande wa Bwana Mc Cain ukisema mgombea wao amemudu zaidi masuala ya usalama wa taifa, wakati wasaidizi wa Bwana Obama wamedai mgombea wao amefaulu mtihani wa kuwa amiri jeshi mkuu kwa kiwango cha juu.

Bwana Obama amesema dola bilioni 700 za mipango ya kuunusuru uchumi wa Marekani ni hukumu ya mwisho kwa utawala wa chama cha Republican.

Amesema Bwana McCain alikuwa amekosea katika suala la Iraq na amemfananisha na Rais Bush. Mgombea wa chama cha Republican Seneta Mac Cain amemuelezea mpinzani wake hana uzoefu wa kuongoza.

Katika mdahalo huo hakuna aliyemuangusha mwenzake, ila maoni ya awali yanaonesha Bwana Obama amefanya vyema zaidi.

No comments: