Thursday, September 25, 2008

Walinda amani washambuliwa Somalia


Mapigano mapya yamezuka Mogadishu mji mkuu wa Somalia, huku majeshi ya kulinda amani ya Umoja wa Afrika yakishambuliwa na wanamgambo wa kisomali.

Raia wasiopungua 15 wameuawa tangu mapigano yalipoanza siku ya Jumanne na idadi kubwa ya watu wamekuwa wakiukimbia mji huo.

Wanamgambo waliwashambuliwa walinda amani wa Umoja wa Afrika kutoka Uganda, ambao walijibu mashambulizi kwa vifaru na mizinga.

Siku ya Jumatatu, watu 30 waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mojawapo ya mapigano makali zaidi kutokea Mogadishu kwa miezi kadhaa.

No comments: