Thursday, September 25, 2008

Wanamgambo wapigwa na jeshi Nigeria


Kundi kuu la wanamgambo wanaopigania mafuta nchini Nigeria limeshutumu jeshi la nchi hiyo kwa kufanya mashambulio ya anga dhidi ya washirika wao.

Movement for the Emancipation of the Niger Delta (Mend), lilitangaza kusitisha mapigano siku tatu zilizopita.Msemaji wa jeshi la Nigeria ameeleza kuwa hana taarifa zozote za mashambulio ya anga kufanyika Jumanne.

Mend limesema lisingependa kutumbukizwa katika mapigano na kuhatarisha mpango wa amani, limedai kuwa litaendelea kutekeleza mpango wa kusitisha mapigano.

Makundi kama Mend yanadai kuwa yanapigani udhibiti wa utajiri wa mafuta kwenye jimbo la Niger Delta ambalo watu wake ni mafukara, lakini kundi hilo linatuhumiwa kwa kujipatia fedha nyingi kutokana na biashara haramu ya mafuta ya wizi.

No comments: