Wednesday, September 24, 2008

Watoto 90 Watekwa Uganda

Umoja wa mataifa umetoa wito kutaka kuchiliwa huru kwa watoto 90 wanaoshikiliwa na waasi wa Uganda kaskazini-mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Unicef imesema ina wasi wasi kuhusu watoto hao, waliotoroshwa kutoka katika shule mbili juma lililopita, kwamba watalamishwa kushiriki katika mapigano ya kivita.

Shirika hilo la kuhudumia watoto la Umoja wa mataifa limesema chifu wa kijiji kimoja pia alitekwa nyara na watu wengine watatu kuuawa.

Kundi la waasi wa LRA limekuwa likifanya maasi kwa zaidi ya miaka 20 ambapo zaidi ya watu milioni mbili wamekimbia makazi yao.

Unicef imesema watoto 50 walitoroshwa kutoka shule moja ya msingi huko Kiliwa na wengine 40 kutoka shule ya sekondari ya Duru katika uvamizi uliofanyika kwa mpigo ndani ya jimbo la Oriental.Pia kijiji kingine cha Nambia, kilishambuliwa.

No comments: