Thursday, October 16, 2008

Shilowa ana chama kipya Afrika Kusini


Wakati mgawanyiko katika chama hicho ulipojitokeza kwa mara ya kwanza, Mosiuoa Lekota, ambaye alikuwa ni waziri wa ulinzi, aligadhabishwa na viongozi ambao sasa ndio wakuu wa chama cha ANC.

Siku saba baada ya hayo, ameweza kutulia. Kundi hili jipya, ambalo bado halijafahamika, lina nia ya kuonyesha kwamba ni chama cha kisiasa ambacho kitaaminika, sio tu mkusanyiko wa wanasiasa walioshindwa vibaya mno.

Mbhazima Shilowa alijiuzulu kama kiongozi wa eneo tajiri zaidi nchini Afrika Kusini la Gauteng, ikiwa ni hatua ya kupinga kuondolewa mamlakani kwa Thabo Mbeki.

Katika mkutano na waandishi wa habari mjini Johannesburg, alithibitisha kwamba anakihama pia chama cha ANC.

Bw Shilowa sasa atashirikiana na Bw Lekota katika kuandaa mkutano wa kitaifa, tarehe 2 mwezi Novemba, chini ya maudhui ''Katika hali ya Kuitetea Demokrasia Yetu''.

Bw Shilowa alisema chama kipya kitajadili mabadiliko ya katiba, na kutokana na yale yaliyompata yaliyompata Thabi Mbeki akiwa rais wa Afrika Kusini, kuamua kama itafaa rais kuchaguliwa na raia moja kwa moja.

Kufikia sasa, Bw Mbeki hajazungumza lolote kuhusiana na chama kipya kilichoanzishwa na rafiki zake.

No comments: