Monday, November 3, 2008

Chama Kipya Chaipa Changamato ANC

Kundi lililojitenga kutoka chama tawala cha Afrika Kusini, African National Congress, ANC linatarajiwa kujiandikisha kama chama.

Chama cha South African Democratic Congress, SADC kinaundwa na waliokuwa wanachama wa ANC waliokihama chama hicho baada ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo Thabo Mbeki kujiuzulu mwezi Septemba.

Katika mkutano wa kitaifa uliofanyika mwishoni mwa juma chama hicho kipya kimekishutumu chama cha ANC kwa kudhoofisha demokrasia nchini humo.

Kiongozi wa ANC, Jacob Zuma amesema anaamini chama chake kitashinda katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.

Chama cha SADC kinaongozwa na Mosiuoa Lekota, aliyekuwa waziri wa ulinzi wa nchi hiyo na mwenyekiti wa ANC.

Naibu wake atakuwa Mbhazima Shilowa, ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu wa jimbo la Gauteng.

SADC inatarajiwa kujiandikisha rasmi kama chama katika tume huru ya uchaguzi nchini humo siku ya Jumatatu.

No comments: