Monday, November 3, 2008

Lipumba: Kikwete Ameonesha Woga


CHAMA cha Wananchi CUF kimesema kuwa kitendo cha Rais Jakaya Kikwete ‘kuyumba’ katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi Oktoba kuelezea kwa ufasaha suala la Tanzania kujinga na Umoja wa Nchi za Kiislamu (OIC) kitaleta mtafaruku nchini. 

Mwenyekiti wa Chama hicho Profesa Ibrahim Lipumba alisema hayo juzi wakati akihutubia maelfu ya wafuasi wa chama hicho kwenye uwanja wa Tropikana,Mabawa jijini Tanga 

Alisema kuwa Tanzania kujiunga na OIC sio jambo la kushangaza kwani taytari nchi 22 zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara zimeshajiunga na umoja huo kutokana na marais wa chi hizo kuridhia. 

Alizitaja baadhi ya nchi hizo zilizojiunga na OIC kuwa ni pamoja na Uganda, Msumbiji, Mali, Togo, Gabon, Senegal, Nigeria, Benini, Burkinafaso na Mauritania. 

“Kwa mfano Uganda na Msumbiji ni miongoni mwa nchi zenye wakristo wengi na hata marais wao ni wakristo lakini wameridhia kujiunga na OIC, kwa nini sisi tusijunge? alihoji, Prof. Lipumba. 

Alisema kuwa katika hotuba yake Rais Kikwete alipaswa awafafanulie vizuri maaskofu waliopinga OIC kwamba haina madhara yoyote na kwamba kuinga huko hakumaanishi kwamba ‘utasilimishwa’ bali ni kuwepo maendeleo ya kiuchumi. 

Aliongeza kuwa Visiwa vya Zanzibar asilimia kubwa ya wananchi wake walisharidhia kujiunga na OIC tangu mwaka 1993 chini ya Rais wa wakati huo, Dkt. Salmin Amour. 

“Rais mwoga katika uamuzi ni hatari sana kwani anaweza kujeta mgawanyiko ndani ya jamii kwa kushindwa kutoa uamuzi katika jambo lililodhahiri,” aliongeza. 

Katika hotuba yake Rais aliwaasa wananchi watulie wakati huu ambapo bado Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje inafanya utafiti kuona faida na hasara za kujiunga na OIC. 

Awali wiki iliyopita, Membe aligusia wakati akizungumza na waandishi wa habari kuwa utafiti umeonesha kuwa OIC ni jumuiya nzuri na kuonya watanzania waache kuwa na woga. Hata hivyo kauli hiyo ilionekana kuwakera maaskofu ambao walimpinga na kumshinikiza ajiuzulu ili "apate mufa wa kushabikia zaidi masuala ya kidini."

No comments: