Friday, November 14, 2008

Majeshi ya kigeni yaonekana Congo.

Ushahidi umeongezeka kwamba kuna majeshi ya kigeni yaliyoingia katika mgogoro wa kivita mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Watu walioshuhudia wameiambia BBC, wamewaona wanajeshi wa Angola na Zimbabwe.

Wakati huo huo waandishi wa habari wametangaza baadhi ya askari wa Jenerali muasi Laurent Nkunda bado wanalipwa mishahara yao na jeshi la Rwanda.

Hii imezusha tena hofu mapigano hayo huenda yakawa kama marudio ya vita vya miaka mitano nchini humo, ambavyo vilihusisha nchi 8 kabla ya kumalizika mwaka 2003.

Watu wapatao 250,000 walikimbia mapigano makali ya hivi karibuni yaliyoanza kupamba moto mwezi Agosti, baina ya majeshi ya Serikali na waasi wanaodai kujilinda dhidi ya waasi wa kihutu kutoka Rwanda waliokimbilia nchini Congo baada ya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.

Wanajeshi hao wanafanya doria lakini hawawezi kuwasiliana na wananchi kwa sababu wanazungumza Kireno.

No comments: