Friday, November 7, 2008

Obama Atazamiwa Kutangaza Baraza Lake

Barack Obama ameanza kuunda serikali yake kwa kumuomba aliyekua mshauri wa Rais Clinton Rahm Emanuel, kuwa mnadhimu wa Ikulu ya Marekani.

Rais mteule Obama anatazamiwa kumteua Waziri wa fedha ambaye jukumu lake kuu ni kukabiliana na hali mbovu ya uchumi.

Licha ya kuanza mapema bado Bw.Obama ana mda hadi tarehe 20 januari mwakani kuchagua baraza lake la mawaziri.

Bw.Obama alichaguliwa kua raia wa kwanza mweusi kuliongoza taifa kubwa duniani akimshinda mpinzani wake kutoka chama cha Republican l John McCain.

Uongozi wa mpito wa Bw.Obama utaongozwa na John Podesta, aliyekuwa mnadhimu wa Ikulu chini ya utawala wa Rais Clinton, pamoja na Pete Rouse, ambaye alikua mnadhimu mkuu wa Seneta wa Bw.Obama.

Hakuna tangazo lolote linalotarajiwa leo alhamisi kuhusiana na shughuli za Bw.Obama lakini wafanyikazi wa Bw.Obama wamesema anatarajiwa kuhutubia wandishi wa habari kabla ya mwisho wa juma hili.

Miongoni mwa nyadhifa kubwa zinazohitajika ni Waziri wa mashauri ya kigeni, Ulinzi na hazina.

Bw.Obama amedokezea kwamba anaweza kumuachia wadhifa wa Wizara ya Ulinzi waziri wa sasa Robert Gates katika moyo ule wa utangamano kama alivyoahidi kuchagua kutoka vyama vyote. Kamanda huyu anasifika kwa mpango wake wa kuongezea idadi ya vikosi nchini Iraq, hatua iliyopunguza ghasia huko.
Mojapo ya ahadi za Barack Obama katika sera yake ya kigeni ni kuyaondosha majeshi ya Marekani huko Iraq katika kipindi cha miezi 18.

No comments: