Friday, November 7, 2008

Wakimbizi Watimuliwa na Waasi Congo.

Mashambulio ya waasi mashariki mwa DR Kongo yamewalazimisha maelfu ya raia wa mji uliokuwa mikononi mwa wanamgambo wanaiunga mkono serikali kuukimbia.

Waasi waliuteka mji wa Kiwanja baada ya siku ya pili ya mapigano na wapiganaji wa kundi liitwalo Pareco Mai-Mai. Baada ya mapigano hayo waasi waliwaamuru raia wa mji huo kuondoka ili wafanye kazi ya upekuzi.

Kiongozi wa waasi Jenerali Laurent Nkunda ameishutumu serikali kwa kuvunja makubaliano ya kusimamisha mapigano yaliyotangazwa wiki iliyopita.

Takriban watu 250,000 wamezikimbia nyumba zao kutokana na mapigano hayo.

Wanawake na watoto ni wengi zaidi walioamriwa kuuhama mji wa Kiwanja siku ya Jumatano.

No comments: