Thursday, November 20, 2008

Wanafunzi wa chuo cha IFM wamevamia wizara ya fedha na uchumi


Wanafunzi wa mwaka wa tatu katika chuo cha usimamizi wa fedha ifm wamevamia wizara ya fedha na uchumi wakipinga kiasi kidogo cha fedha kilichotolewa na serikali kwa ajili ya chakula na malazi baada ya kutolipwa kwa takribani miezi miwili. 

Wakiwa wamesimama katika lango kuu la kuingilia katika ofisi za wizara hiyo wanafunzi hao wamedai kuwa kiasi cha shilingi millioni 1 kilichotolewa na wizara hiyo kwa kila mwanafunzi badala ya million 1 na laki 3 hakikikidhi gharama za maisha kutokana na wafunzi wengi kuwa na madeni yaliyotokana na kucheleweshwa kwa malipo na wizara hiyo. 

Aidha ITV ilimtafuta msemaji wa wizara ya fedha na uchumi ili kuzungumzia tatizo hilo bila mafanikio na baadhi ya wafanyakazi waliokwepo katika jengo hilo walidai kuwa yuko katika mkutano.

*Source ITV Medeia*

No comments: