Friday, November 21, 2008

...Mahakimu Washitaki kwa IGP


MAHAKIMU wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambao hivi karibuni waliripotiwa kulazimika kuomba kuhakikishiwa usalama wao kwa viongozi wa Idara ya Mahakama nchini kutokana na kutishwa na baadhi ya vigogo wa EPA ambao kesi zao zimefunguliwa mahakamani hapo. 

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam jana, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema alithibituisha mahakimu hao kulalamika na jeshi lake limekwishayapokea malalamiko hayo na kuahidi kuyafanyia kazi. 

IGP Mwema alisema, bila kuwataja mahakimu waliolalamika, vitisho hivyo vilianza dhidi ya mahakimu na waendesha mashitaka wa kesi hizo mara tu baada ya washitakiwa mbalimbali kuanza kusimamishwa kortinini hapo. 

"Ni kweli tumepokea malalamiko kutoka kwa mahakakimu na waendesha mashitaka wa kesi za EPA na kwamba tunayafanyia kazi ila tumewahakikishia usalama wao," alisema. 

Aliongeza kuwa mpaka sasa hakuna mtu aliyekamatwa kuhusika na utoaji wa vitisho hivyo kwa mahakimu na waendesha mashitaka hao. 

Akizungumzia juu ya watuhumiwa wengine wa sakata hilo wanaotarajiwa kufikishwa mahakamani alisema suala hilo lipo kwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) ambaye amekabidhhiwa ripoti ya uchunguzi juu ya suala hilo. 

Alisema kuwa wao wakiwa Jeshi la Polisi wataendelea kutoa ushirikiano unaohitajika juu ya uendeshaji wa kesi hizo pale watakapohitajika. 

"Sisi tukiwa Jeshi la Polisi tuliteuliwa katika Tume ya Uchunguzi na ripoti tayari ipo kwa DPP, hivyo kama kuna lingine linalohitajika kuhusu hili, tutaendelea kutoa ushirikiano wetu," alisema IGP alipokuwa akijibu swali kuhusu suala hilo la kashifa ya EPA. 

IGP Mwema ni mmoja wa wajumbe katika Timu Maalum iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete ambayo ilipwa jukumu la kuipitia ripoti ya wakaguzi wa Ernst and Young na kutoa mapendekezo yao juu ya namna ya kuwachukulia hatua washitakiwa waliohusika na ufisadi kwenye akaunti ya EPA. 

Wajumbe wengine kwenye kamati hiyo ni Mwanasheria Mkuu, Bw. Johnson Mwanyika ambaye pia ni Mwenyekiti na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rsuhwa (TAKUKURU), Dkt. Edward Hosea.

No comments: