Sunday, September 28, 2008

Atimaye Serikali Yalainika Kwa NMB

BAADA ya serikali kupiga chenga tangu Agosti 28 kusaini mkataba wa malipo ya mkupuo na maslahi mengine, serikali jana ilisalimu amri kwa wafanyakazi wa benki ya NMB iliposaini mkataba huo, lakini shughuli ya kusaini ikiwa imetanguliwa na mvutano mkubwa.

Uamuzi wa kusaini umefikiwa na serikali baada ya wafanyakazi hao kugoma kwa siku mbili na kusababisha adha kubwa kwa wateja wa benki hiyo, wengi wakiwa wafanyakazi wa serikali, wakiwemo wa taasisi nyeti kama jesi, Polisi na halmashauri.

Kipengele hicho kinaeleza kuwa hisa za wafanyakazi zitakuwa zinasimamiwa na hazina badala ya makubaliano ya awali kuwa hisa hizo zisimamiwe na wafanyakazi wenyewe kupitia Tuico-chama cha wafanyakazi wa viwandani na taasisi za fedha.

“Msiturudishe nyuma... haya mambo tulishayajadili siku nyingi chini ya wanasheria na tukakubaliana na kilichotuleta hapa leo ni kutiliana saini tu, si kuendelea kujadili suala hili,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao.

“Hatukitaki kipengele hicho kiondolewa kwanza kwa sababu mwanzo hakikuwepo mmekiingiza kiujanja ujanja na ndiyo maana mmeleta mkataba huu dakika za mwisho. Sasa msimamo wetu ni kwamba hatukitaki la sivyo hatusaini.”

No comments: