Sunday, September 28, 2008

Kifo Cha Wangwe Chageuka Dili Kampeni za Tarime

MAMBO yanayojitokeza katika kampeni za uchaguzi mdogo wa Tarime yanazidi kuvuruga amani na utulivu yakionyesha wazi kuwa kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Chacha Wangwe ni mtaji mkubwa wa kisiasa.

Tangu kufariki dunia kwa mwanasiasa huyo machanchari katika ajali ya gari katika eneo la Pandambili, wakati akitoka Dodoma kuelekea Dar es Salaam, mambo mengi yamekuwa yakijitokeza katika sura ya kutaka kukitumia kifo hicho kama ngazi ya kupandia kisiasa na na kujiongezea umaarufu wa kushinda jimbo hilo.

Dalili za kwanza kabisa za kutumia msiba huo kama mtaji, zilijionyesha katika kampeni za mgombea wa CCM, ambapo mmoja wa ndugu wa marehemu Wangwe alisimama kwenye jukwaa na kutoa tuhuma za wazi za kukihusisha kifo cha ndugu yake na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Katika hali inayodhihirisha kuwa kifo hicho kishikiwa kidedea kuwavusha watu kisiasa, hata vyama vingine, kikiwamo cha Demokratic Party cha Mchungaji Chritopher Mtikila vimeanza kutumia agenda ya kifo cha Wangwe kama panga la kuwakata makali Chadema.

No comments: