Tuesday, September 30, 2008

Kongo Yajibu Shutuma za Askari Watoto

Waziri kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametoa changamoto kwa ripoti iliyotolewa juu ya ongezeko la kuingiza watoto jeshini na vitendo vya ubakaji mashariki mwa nchi hiyo.

Waziri wa ulinzi, Chikez Diemu, alisema serikali inatatua matatizo hayo kwa kuwakamata washukiwa na kuwafikisha katika mahakama za kijeshi.

Ripoti iliyotolewa na shirika la kimataifa la Amnesty imesema kwa kila askari watoto wawili walioachiliwa huru, watano hurejeshwa tena katika jeshi hilo.

Mifano ya watoto hao waliotolewa mfano katika ripoti hiyo ni kutoka jimbo la Kivu kaskazini.

Ilisema baadhi ya askari hao watoto walioruhusiwa kwenda kwao walichukuliwa tena na makundi ya watu wenye silaha.

Jeshi la Kongo limekuwa likipigana na wapiganaji wanaomtii Jenerali Laurent Nkunda mashariki mwa nchi hiyo.

Mapigano hayo yamesababisha maelfu ya watu kuhama makazi yao.

No comments: