Thursday, November 20, 2008

Juma Nature Ageuka Kivutio Kizimbani

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Temeke jana, ilisheheni umati wa watu, wakiwemo wazazi wa Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya ( Bongo fleva) jijini Dar es Salaam, Juma Kassim Nature, (28) akikabiliwa na tuhuma za kumbaka Mwanafunzi wa Kidato cha tatu (16) kwa zamu.

Tuhuma hiyo, inamuhusisha pia Godwine Malima (26), ambaye ni Mwalimu anayekabiliwa na tuhuma za kumbaka mwanafunzi huyo na kumchukua kwenda kuishi naye kinyume na ridhaa ya wazazi.

Hata hivyo Nature, alifikishwa mahakamani hapo, akiongozwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke Emmanuel Kandihabi, majira ya saa 4:15, alipokuwa akishikiliwa na hatiani katika kituo cha Changombe cha Wilaya hiyo.

Aidha mara tu baada ya kumfikisha mahakamani hapo, Kandihabi, alisisitiza kuwa ni lazima msanii huyo, asomewa mashtaka yake leo, ili hatua za kisheria zichuke mkondo wake.

Mara baada ya msanii huyo kufikishwa mahakamani hapo, na mwenzie kwa ajili ya kusomewa mashtaka yanayo wakabili, mahakama ilionekana kujaa na umati mkubwa uliokusanya watu mbalimbali wakiwemo wasanii wake pamoja na familia yake.

Hata hivyo, msanii huyo alipandishwa kizimbani majira ya saa 8:15 kwa ajili ya kusomewa shataka la kubaka linalomkabili, akiwa amaeambatana na mshtakiwa mwenzie ambae anakabili na tuhuma za kumchukua mwanafunzi huyo na kwenda kukaa naye kinyume na ridhaa ya wazazi wake.

Aidha Mwendesha Mshtaka, Mrakibu wa Polisi Basill Pandisha, alisema kuwa washtakiwa hao, walitenda kosa hilo mnamo Novemba 1 mwaka huu eneo la Sugar Rays, jijini Dar es Salaam, na kudai kuwa, mtuhumiwa namba moja ambaye ni Juma Kassim alimbaka mwanafunzi huyo bila ya ridhaa yake, huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Ilidaiwa katika maelezo ya malalamikaji kuwa, mnamo majira ya saa 1:40 usiku maeneo ya Sugar Rays, mlalamikaji alikuwa ameenda kwa mtuhumiwa kwa lengo la kuzungumza naye, kwani wiki mbili zilizopita mtuhumiwa alikuwa akimsumbua kupitia namba yake ya simu.

Ilielezwa kuwa, mlalamikaji alipofika nyumbani kwake alimkuta rafiki yake Godwine Malima ambaye ni mshtakiwa wa pili na kudai mtuhumiwa hayupo hivyo aliamua kumsubiri.

Hata hivyo ilielezwa kuwa, wakati mlalamikaji akiendelea kumsubiri ghafla mtuhummiwa namba mbili, alimwambia mwanafunzi huyo, waende naye na walifikia katika vyumba vya kulala wa geni, iliyoko Sugar Rays, ndipo alipofika Juma Kassim na kuzungumza naye.

Katika kosa la pili Pandisha aliieleza mahakama kuwa mnamo mmuda na majjira yanayofanana, mshtakiwa namba mbilii, Godwine Malima, anatuhumiwa kintume nasheria kumchukua mlalamikaji huyo, na kwenda naye nyumbani kwake, bila ya ridhaa ya wazazi wake, huku akijuafika kuwa ni mwanafunzi na anaumri wa miaka chini ya 18.

Watuhumiwa kwa pamoja walikana shtaka hilo, na kupewa dhamana kwa mmasharti ya kuleta mdhamini mmoja mwenye mali isiyo hamishika, na mfanyakazi wa serikali kwa dhamana ya shs. 5 milioni.

Hata hivyo, mtuhumiwa namba moja, Juma Kassim alipewa dhamana baada ya kuweza kutimiza masharti ya dhamana, huku mwenzie akionekana kusuasua baada ya wadhamini wake kutokuleta barua ya dhamana.

Hakimu Riwa, alimwambia mtuhumiwa namba mbili,, mahakam iko tayari kumsubiri wadhamini wafuatilie kitambulisho pamoja na barua ya udhammni inayoonyesha kweli maeajjiliwa na Serikali, n aakichelewa atlazimika kwenda mahabusu.

Baada ya kusomewa mashtaka watuhumiwa hao, na kupewa dhamana, kwa Juma Nature, Mwanachi ijaribu kuzungumza na Wazazi wake lakini walionekana kujawa na simmanzi kubwa na hawakuwa tayari kuzungumza lolote.

Aidha , Mwananchi haikukata tamaa, baada ya wazazi hao, kukataa kabisa kuzungumza na waandishi,bbali irusha tena kombola kwa wasanii wenzie waliokuwa wafika mahakamni hapo kwa ajili ya kuju hatma ya Kamanda wao katika fani ya muziki, na pia walionyesha kukataa kabisa kuzungumza.

Hata hivyo alisikika msanii mmoja miongoni mwao, alimkazia macho Mwandishi wa hababri hizi, na alipoulizwa swali alisikika akijibu kuwa unataka kujua jina langu ili iweje , na kuonyesha kukerwa na swali lile na kuendelea kuongea kwa ukali huku akimuuliza, unanijua mie ni nani, sina muda wa kuzungummza nawe alidai msanii huyo.

2 comments:

Anonymous said...

Juma Nature ajiweke katika viatu vya huyo mtoto angekuwa ni yeye kafanyiwa unyama huo angejisikiaje?? Na kwanini umfanyie binadamu mwenzio unyama huo??? Kwakweli anastahili adhabu sio vizuri kabisa huo ndio tunauita UKATILI KWA WANAWAKE

Anonymous said...

unao uhakika kama kafanya kweli kitendo hicho?..kama ni kweli anastahili adhabu kama watu wengine..kama kasingiziwa itakuwa kafanyiwa yeye kosa na huyo mutu anastahili adhabu pia.